Wednesday, April 1, 2015



QUALITY ANIMAL FEEDS

Chakula cha kuku na ng’ombe cha KIBOKO ni chakula chenye Ubora wa hali ya juu na kinatengenezwa kwa kuzingatia maadili yote ya Uzalishaji yanavyopaswa kutekelezwa.

Aina ya vyakula:
1.     Kuku wa nyama (Broilers):
BROILER STARTER
BROILER FINISHER

2.     Kuku wa mayai (Layers):
CHICK MASH
GROWERS MASH
LAYERS MASH

3.     Dairy Meal (Ng’ombe wa Maziwa):
Matumizi:
1.     Kuku wa nyama (Broilers):
Broilers- watachukuwa muda wa takriban wiki NNE pekee wakilishwa chakula cha KIBOKO ANIMAL FEEDS.
Chakula- wiki 1-2.5 wape Broiler Starter bila kuwapimia na maji safi ya kunywa ya kutosha.
-  wiki 2.5-4 wape Broiler Finisher mpaka washibe na pia maji safi wakati wote.
ZINGATIA CHANJO NA USAFI WA BANDA NA MAZINGIRA IPASAVYO KWA MATOKEAO BORA NA FAIDA.
2.     Kuku wa mayai (Layers):
Layers – watachukua muda wa kati ya wiki 16 hadi 20 kuanza kutaga.
Chakula- wiki 1 – 6 wape Chick Mash ya kutosha na maji safi.
              -Wiki 6 – 16 wape Growers Mash ya kutosha na maji safi ya kunywa kila wakati.
              - Wiki 16 na kuendelea wape Layers Mash kwa ajili ya kuanza kutaga na kuendelea                                                                                   pamoja na maji safi ya kunywa kila wakati.
CHANJO NA USAFI NI MUHIMU SANA KWA MATOKEO BORA KWA UFUGAJI WA FAIDA.
MAMBO MUHIMU:
ü  Zui watu wasiohusika, kuku na ndege kuingia au kukaribia mabanda yako.
ü  Hakikisha banda lipo katika mazingira safi yasiyofurika au kutuama maji.
ü  Ondoa mbolea mara kwa mara ikiwa ndani ya mifuko na tupa mbali na eneo la mabanda.
ü  Wafanyakazi wote wabadilishe nguo na wawe safi. Wasafishe mikono na miguu yao kila wakati waingiapo mabandani kwa kutumia dawa.
ü  Dawa ikwekwe kwenye maji ya mlangoni ili kutumbukiza  miguu kabla ya kuingia bandani na kubadilishwa kila wiki.
ü  Mabanda yapumzishwe wiki mbili kabla ya kuwekwa kuku wapya.
ü  Kabla ya kuweka kuku wapya, safisha mabanda kwa kutumia dawa na ufunge banda kwa muda wa siku saba.


JINSI YA KUSAFISHA NA KUPIGA DAWA MABANDA KABLA YA KUINGIZA KUKU (FUMIGATION)
Ondoa mbolea na vitu vyote vilivyotumika (mifuko ya chukula, makopo, n.k) na kuitupa mbali kabisa na mabanda yako.
ü  Anza kusafisha dari, halafu kuta na kumalizia na sakafu.
ü  Loweka vyombo vya kunywea maji  na kulishia chakula na vifaa vyote vinavyotumika ndani  ya mabanda kwenye dawa kwa muda wa nusu saa halafu suuza na maji ya kawaida.
ü  Piga dawa ya wadudu warukao na watambaao ndani na nje ya banda.
ü  Weka dawa kwa FOOTBATH… mlangoni kabla ya kuleta vifaranga.

KUDHIBITI KUSAMBAA MAGONJWA NDANI YA MABANDA.
ü  Osha vyombo vya kunywea maji kila unapoweka maji mpya.
ü  Loweka vyombo kwenye dawa kwa muda wa nusu saa angalau mara moja kwa wiki.
ü  Badili maji yenye dawa mlangoni  mara moja kwa wiki.
ü  Kama unatumia maji yasiyo salama, weka dawa ya kuua vimelea vya magonjwa. Kumbuka maji salama kwa kuku ni yale ambayo hata wewe mfugaji unaweza kuyanywa.
ü  Jiepushe na vyakula vyenye mahindi na dagaa walihoribika kwa sababu ni chanzo cha sumu ya mycotoxins ni hatari kwa kuku.

MAGONJWA YA KUKU WA MAYAI.
NA.
MAGONJWA
DALILI
CHANJO/TIBA
1.
New Castle Disease (Mdondo).
-   Vifo vingi vya ghafla.
-   Kuharisha.
-   Hutokea wakati wowote baada ya wiki mbili.
Chanjo siku ya 7, rudia siku ya 21 kila baada ya wiki 12.
2.
Gumboro.
-   Vifo vya ghafla
-   Kukunja mabawa chini.
-   Kujikusanya pamoja.
-   Kuharisha kinyesu cheupe.
-   Ugonjwa hutokea kuanzia wiki ya 2 hadi 18.
Chanjo siku ya 10 – 14, rudia siku ya 28 na 42 kwa kuku wa mayai.
3.
Avian Leukosis Complex.
-    Mavecks – humpata kuku kuanzia umri wa wiki tatu, lakini mara nyingi ni wiki ya 12 – 24.
-    Dalili ni kupooza mabawa, kuvimba na kufa.
-    Kuvimba miguu, maini, wengu na figo.
Tibu.
4.
Fowl Typhoid (kideli).
-   Vifo vya kuku mmoja mmoja.
Tibu.
5.
Pollorum.
-   Huuwa zaidi vifaranga wadogo kuanzia siku ya kwanza hadi wiki tatu.
-   Vifaranga hujikusanya karibu na chanzo cha joto na kusinzia na kutoka na uharo mweupe.
Zingatia usafi wa mabanda na tiba.
6.
Paratyphoid.
-   Dalili hazionekani, vifo hutokea wiki ya kwanza vifaranga hudumaa, wachovu na wanaweza kuharisha.
Tibu.
7.
Colibacilosis.
-   Vifo wiki ya kwanza vitovu havikauki.
-   Hushindwa kupumua.
-   Macho na kichwa kuvimba.
-   Tumbo hujaa maji (Ascitis).
Tibu.
8.
Colyza (majua)
-   Kupiga chafya.
-   Kutoa makamasi.
-   Kuvimba uso mara chache na kupata pneumonia.
Tibu.
9.
Coccidiosis (kuharihsa damu)
-    Dalili zipo nyingi.
-    Kinyesi kuwa na rangi ya ugoro au damu tupu.
-    Vifaranga kudumaa.
Tibu.
10.
Foul Pox (Ndui).
-   Kwa kuku wa mayai.
Kila kuku atachinjwa sahemu katika mbawa. Endelea kuwapa maji ya vitamin.

MAGONJWA YA KUKU WA NYAMA:
NO.
MAGONJWA
DALILI
CHANJO/TIBA.
1.
New Castle (Mdondo).
-   Vifo vingi vya ghafla.
-   Kuharisha
-   Hutokea wakati wowote baada ya wiki mbili.
Chanjo kwa masaa wawili tu endelea na maji ya vitamin wiki ya kwanza.
2.
Gumboro.
-   Vifo vya ghafla.
-   Kukunja mabawa chini.
-   Kujikusanya pamoja.
-   Kuharisha kinyesi cheupe.
-   Ugonjwa hutokea kuanzia wiki ya pili.
Chanjo kwa masaa mawili tu na endelea na maji ya vitamin.

MAGONJWA YA MLIPUKO:
·         New Castle (Mdondo).
·         Gumboro.


3.     KIBOKO Diary Meal:
Chakula bora cha ng’ombe wa maziwa. Kilo sita (6) tu kila siku zinatosha kumfanya ng’ombe wako atoe maziwa mengi na ya kutosha.
·         Mpe kilo tatu (3) asubuhi na tatu (3) jioni wakati wa kukamua.
·         Ng’ombe ale majani ya kutosha na apewe maji safi na salama ya kunywa.
·         Ng’ombe apate chanjo kwa ajili ya magonjwa ya mlipuko.
·         Mwogeshe ng’ombe wako mara kwa mara kwa kutumia dawa.
·         Ng’ombe alale mahali pazuri na pakavu.

ANGALIZO:
        I.            Ng’ombe apate tiba kwa wakati.
      II.            Ng’ombe apate dawa ya minyoo kwa wakati.



KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI:

Ø  Sai Energy and Logistic Services,
P.O.Box 333, Iringa, Tanzania.
Ø  Tel:-           : (026) 2725039, (026) 2725053
Ø  Mobile      : 0712604888, 0763299664, 0786870697.
Ø  Fax             : (0260 2725004.
Ø  Email:-      : saienergy@motomoto.co.tz


No comments:

Post a Comment