SOMO 1 UTANGULIZI
FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU
a) Chakula – nyama ya kuku na mayai hutumika kama Chakula
minimum cha wanadamu
b) Chanzo cha kipato – Mkulima hupata fedha akiuza kuku
au mayai
c) Chanzo cha ajira – ufugaji wa kuku hutoa ajira kwa
jamii
d) Mbolea – kinyesi cha kuku kinaweza kutumika katika
kurutubisha mashamba ya mazao
e) Shughuli za utafiti – kuku wanatumika katika tafiti
nyingi za Baiologia kama kutambua mambo ya lishe.
f) Shughuli za viwandani:
·
Mayai
yenye mbegu ya jogoo hutumika katika kutengeneza dawa za chanjo
·
Magamba
ya mayai yanaweza kutumika katika utengenezaji wa vyakula vya wanyama
·
Kiini
cha njano cha mayai kinaweza kutumika kutengenezea mafuta ya kuoshea nywele
(shampoo0
g) Kutunza kuku kwaajili ya kizazi kijacho ili kizazi
kijacho kiweze kuona kuku ni lazima hivi sasa waendelee kufugwa.
VIKWAZO KATIKA UFUGAJI KUKU
a) Chakula mara nyingi vyakula vya kuku vinakuwa vyenye
ubora hafifu na hata upatikanaji wake huwa si mzuri
b) Magonjwa – magonjwa kama mdonde au ndui huathiri
ufugaji wa kuku. Ni vema magongwa kama hayo yakingwe au kuzuiwa ili kuendeleza
ufugaji
c) Mtaji – mara nyingine mtaji huwa kikwazo lakini endapo
mikopo midogo midogo itatolewa kwa vikundi vitakavyo kuwa tayari na ufugaji
utaendelezwa
d) Madawa ya kuku – gharama za madawa ya kuku ziwe chini
ili kuendeleza ufugaji.
e) Tabia na miiko ya Jamii – baadhi ya jamii za makabila
hapa chini, ufugaji wa kuku huona kama ni kitu duni hivyo basi jamii hizo
zishawishiwe ili ziweze kuweka mkazo katika ufugaji wa kuku kwa nia ya
kujiongezea kipato na kupata lishe bora pamoja na ajira.
SOMO LA 2 SIFA ZA KUKU WA KIENYEJI
SIFA
1.
Wana uwezo wa
kuatamia mayai yao na kuangua vifaranga
2.
Wana uwezo wa
kujitafutia Chakula ardhini lakini ili kuwaendeleza ni minimum wakaandaliwa
Chakula bora na cha kutosha.
3.
Wana uwezo wa
kujilinda na maadui zao kama mwewe
4.
Wavumilivu wa
magonjwa mengo ya kuku lakini ni minimum wakikingwa na baadhi ya magonjwa ya
kuku kama mdonde, ndui ya kuku
Ili kuweza kuwaendeleza:
Ni minimum kuku wao wakapewa mafunzo mazuri. Wawekwe kwenye mabanda
mazuri wapewe maji na Chakula cha kutosha.
SOMO LA 3 MFUMO YA KUZALISHA KUKU
A: Mfumo wa ufugaji huria
Huu ni mfumo rahisi lakini si mzuri kwa mfugaji wa kuku wengi kwani
atahitaji eneo kubwa la ardhi. Katika kutumia mfumo huu kuku hufugwa ndani
wakati wa usiku na kuachiwa huru wakati wa mchana ili kujitafutia Chakula.
Faida zake:
1.
Gharama ndogo za
ujenzi wa nyumba.
2.
Gharama za Chakula
hupungua kwani kuku huokota wadudu na kula baadhi ya majani
3.
Gharama za kujenga
uzio hazihitajiki
4.
Kuku wa aina au umri
wowote wanaweza kufugwa kwa mfumo huu.
Hasara za mfumo huu:
1.
Uwezekakano mkubwa
wa kuku kuliwa na vicheche au kuibiwa mitaani na kukanyagwa na magari
2.
Kuku hutaga popote
na upotevu wa mayai ni mkubwa
3.
Kuna usimamizi
hafifu wa kundi la kuku
4.
Ni rahisi kuku
kuambukizwa magonjwa ya kuku
5.
Utagaji unakuwa si
mzuri kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa
6.
Uwekaji wa
kumbukumbu si mzuri na mara nyingi kumbukumbu si sahihi.
Utumiaji mzuri wa mfumo huu:
1.
Wajengee banda kuku
kwa ajili ya nyakati za usiku na endapo hali ya hewa inakuwa si nzuri
2.
Kuku wapatiwe
Chakula na maji
3.
Kuku wapatiwe viota
vya kutagia
4.
Kuku 100 watumie
eneo la ardhi la ½ ha.
MFUMO WA NUSU NDANI NA NUSU NJE
Katika kutumia mfumo huu kuku huwekwa kwenye mabanda yenye hewa ya
kutosha na kuwe na uzio wenye majani. Uzio unaweza kujengwa kwa kutumia nyaya
zenye matundu au miti.
FAIDA ZA MFUMO HUU:
1. Tabia mbaya za kuku kama vile kudonoana si nyingi
2. Mfumo huu hutumika kwa kuku wenye umri wowote
3. Utunzaji wa kuku ni rahisi ukilinganisha na ule wa
huria
Hasara za mfumo huu:
1. Unahitaji gharama za uzio
2. Si nzuri kwa kuku wa nyama
3. Matumizi ya muda mrefu ya eneo husika laweza kuwa na
minyoo au vemelea vingine vyovyote vya magonjwa
Utumiaji mzuri wa mfumo huu
1. Fanya usafi wa eneo husika na banda kila siku
2. Ikiwezekana kuwe na mzunguko wa kutumia eneo hilo
c. MFUMO WA KUTUMIA MABANDA YENYE MATANDIKO:
Katika kutumia mfumo huu kuku huwekwa kwenye mabanda ambayo yana sakafu
au la, eneo la ndani hufunikwa na matandiko ya makapi ya mpunga, au takataka za
mbao au maganda ya karanga.
FAIDA ZA MFUMO HUU
1. Ni mzuri kwenye maeneo yenye ardhi haba
2. Uangalizi wa kuku ni mzuri na ni rahisi
3. Mchanganyiko wa vitamin B hutengenezwa katika
matandiko hayo
4. Hakuna haja ya kufagia vinyesi vya kuku kila siku
5. Joto litokanalo na matandiko lina uwezo wa kuuwa
vimelea vya maradhi
6. Kuku wanakingwa na hali ya hewa mbaya na maadui
wengine
7. Ni rahisi kukinga maradhi ya kuku
8. Uwekaji wa kumbukumbu ni rahisi
HASARA ZA MFUMO HUU
1. Uwezekano wa kuku kudonoana ni mkubwa
2. Gharama za ujenzi wa mabanda zinahitajika
UTUMIAJI MZURI WA MFUMO HUU:
1. Matandiko yageuzwe kila siku
2. Sehemu ya matandiko iliyomwagikiwa na maji izolewe
3. Kila mara matandiko yawe makavu kwa kuwa na madirisha
yanayopitisha hewa ya kutosha ambayo itatoa unyevu nyevu, hewa chafu pamoja na
ammonia
4. Mita mraba moja hutosha kwa kuku 5-8
Dhumuni kuu ni kupata kundi la kuku litakalofaa kwa
sifa zote katika uzalishaji
Vipengele vya kuzingatia katika kuchagua kuku:
·
Utoaji wa mayai kwa
mwaka uwe mzuri
·
Umbile la mwili na
jinsi aonekanavyo
·
Uvumilivu wa
maradhi, hii ni sawa na kuwa na vifo vichache
·
Uwezo wa kuotesha
manyoya haraka
·
Uwezo mkubwa mwilini
wa kutengeneza Chakula kuwa mayai au nyama
·
Ulaji wa Chakula uwe
mdogo ukilinganisha na uzalishaji wake
·
Utagaji uwe wa muda
mrefu kabla ya kupumzika
·
Uwezo wa kuatamia na
kuangua vifaranga wengi na kuwalea
Njia zitumikazo katika kuchagua
·
Kwa kuangalia kuku
wenyewe kulingana na sifa zilizotajwa hapojuu
·
Kwa kufuatilia
kumbukumbu za wazazi wa kuku unaotaka kuwachagua
·
Kwa kuangalia
kumbukumbu za familia (kaka na dada)
KUCHAGUA KUKU WASIOFAA KWENYE KUNDI
·
Inasaidia kuongeza
uzalishaji wa mayai
·
Inapunguza kulisha
kuku ambao uzalishaji wake ni hafifu
·
Inapunguza uenezaji
wa magonjwa ya kuku
·
Huongeza nafasi
zaidi kwa kuku wazuri kwenye banda
·
Uwezekano wa kuuza
kuku kama hao ni mkubwa kabla hawajafa.
LINI KUCHAGUA?
·
Mara tu wakitotolewa
·
Wakati wa ukuwaji
·
Shughuli ya kila
siku
·
Kuku waanzapo kutaga
·
Uzalishaji ukishuka
chini ya asilimia 50
·
Wakati kuku
wakiangusha manyoya
UPANDISHAJI WA KUKU
·
Kuku wenye uzito
mdogo temba 15 hadi 20 kwa jogoo mmoja
·
Kuku wenye uzito wa
juu temba 10 hadi 15 kwa jogoo mmoja
MIFUMO YA UPANDISHAJI
·
Upandishaji wa kuku
wa koo moja au walio karibiana kiuzawa
·
Upandishaji wa kuku
wa koo au jamii tofauti
·
Uboreshaji wa kuku
wa kienyeji kwa kutumia majogoo ya kisasa. Lengo ni kuhamisha sifa nzuri za
jogoo kwa vizazi vifuatavyo.
Huu ni uanguaji unaofanywa na kuku kwa kuatamia mayai. Kwa kawaida kuku
mmoja anaweza kuatamia mayai 12 hadi 15 kwa mara moja. Kuku awekewe mayai ya
kuanguliwa wakati wa kuatamia ukifika.
FAIDA ZA UANGUAJI WA ASILI WA VIFARANGA
(i)
Mashine za kuangulia
hazihitajiki hivyo gharama yake huwa ni kidogo
(ii) Mfugaji hahitaji ujuzi maalumu katika kufanya shughuli
hii.
(iii) Huhitaji kuchunguza sehemju za ndani za mayai kwa
kutumia mwanga kama inavyofanyika katika uanguaji kwa kutumia mashine.
(iv) Huhitajiki kurekebisha joto, unyevunyevu. Hali ya hewa
na hata kugeuza mayai kama inavyofanyika kwenye mashine
(v) Huhitaji kuajiri mtu wakati unatumia uanguaji wa asili
wa vifaranga.
KUCHAGUA MAYAI KWA AJILI YA UANGUAJI WA ASILI WA
VIFARANGA
Uanguaji huboreshwa zaidi kwa kuzingatia uchaguzi wa mayai yanayofaa kwa
kutotolewa, epuka mayai yafuatayo:
1.
Mayai madogo sana
2.
Mayai yasiyo na
umbile la kawaida
3.
Mayai yenye mafuta
matuta
4.
Mayai yenye viini
viwili vya njano
5.
Mayai yenye matundu
matundu mengi
6.
Mayai ambayo hayana
mbegu ya jogoo
7.
Mayai yaliyotoka
kwenye kundi la kuku waliozeeka mno
8.
Mayai kutoka kwenye
kuku wagonjwa
9.
Mayai
yaliyohifadhiwa visivyo
10.
Mayai kutoka kwenye
mitetea yenye majogoo machache kuliko inavyoshauriwa.
Matayarisho yakiota
Kiota kitayarishwe kabla ya kuku hajaanza kutaga. Ndani yak iota weka
matandiko kiota kiwe safi na kinyunyuziwe dawa ya unga (sevin) ya kuua wadudu.
Kila baada ya kuangua kiota kisafishwe kabla ya kutumika kwa kuku wengine.
Kumtayarisha kuku wa kuatamia
Kuku wanaotazamiwa kuatamia ni lazima wachunguzwe kwa makini siku mbili
kabla ya kuatamia ili kuhakikisha kwamba hawana chawa. Utitiri au viroboto.
Kuwepo kwa wadudu hao huwafanya kuku wakose raha na wasitulie kwenye viota vyao
hali hii husababisha kuanguliwa kwa vifaranga wachache. Ikiwa kuku wana wadudu
hao wanyunyize dawa. Kuku kwa ajili ya kuatamia awe na tabia na uwezo wa
kuatamia na kuangua vifaranga vingi.
Uwezo kutumia boksi au kikapu kutengeneza kiota cha kutamishia
Faida
·
Vifaranga vingi
huweza kutotolewa kwa wakati mmoja
·
Joto, unyevu pamoja
na hewa hudhibitiwa
·
Hali ya usafi ni
nzuri
·
Mayai yasiyofaa
yanaweza kutolewa wakati wowote kabla ya siku ya kutolewa vifaranga.
·
Vifaranga hupatikana
kwa mpangilio
Hasara
·
Gharama za kuanzia
na kuendeshea ni ghali
·
Ujuzi maalumu
unahitajika
·
Uwezekano wa
milipuko ya magonjwa upo endapo mayai yatatoka kwenye vyanzo vingi
·
Uzalishaji unaweza
kusimama endapo mashine itaharibika
·
Kutakuwa na gharama
za ujenzi wa nyumba kwa ajili ya kuwekea mashine
Mahitaji minimum katika kutotoa mayai kwa kutumia mashine
1. HALI YA JOTO
Joto linalohitajika kwenye mashine ni kati ya nyuzi 370c had 39Oc
2. UNYEVUNYEVU
Yai linaweza kupoteza unyevunyevu kati ya asilimia 11 hadi 13 wakati
liko kwenye mashine. Hivyo basi ili kuzuia maji mengi yasipotee kwenye yai ni
lazima kwenye mashine kuwe na kifaa cha kuwekea maji. Unyevunyevu unaohitajika
kwenye mashine ni asilimia 70 – 75 hadi siku ya ishirini na kupunguzwa hadi
asilimia 50 baada ya vifaranga kuanguliwa ili vipate kukauka.
3. HEWA SAFI
Kunatakiwa kuwe na chanzo cha hewa safi kwa ajili ya mayai yaliyomo
kwenye mashine. Panga boi au matundu hutumika kwa shughuli hii
4. Kugeuza mayai
Mayai hugeuzwa kwa siku 18 za kwanza. Lakini yasigeuzwe kwa kipindi cha
masaa 24 ya kwanza. Mashine ambazo zina kifaaa cha kugeuza mayai pekee hugeuza
mayai kila baada ya saa moja lakini ugeuzaji wa mayai kwa mikono hufanyika mara
tatu au tano kwa siku.
Kuchagua vifaranga
Baada ya vifaranga kutotolewa inabidi kuchagua vifaranga ambavyo havina
dosari. Vifaranga vyenye dosari vitolewe navyo ni vile ambavyo ni vidogo sana
vilema na vile vyenye vitovu vibichi
Kufusha mashine za kutotolea
Ili kuua vimelea vya maradhi mashine za kutotolea hufushwa baada ya
kusafishwa na wakati wa kuweka mayai mapya. Lakini usifushe mashine mnamo saa
96 (ambavyo ni sawa na siku nne) baada ya kuweka mayai kwenye mashine, kwani
huu ni wakati ambao moyo wa kifaranga unaanza kufanya kazi. Tumia gram 114 za
formalin kwa gram 85 za potassium permanganate katika kila ujazo wa mita 3
(3m2) za mashine.
Maandalizi minimum kabla ya kutunza au kupokea
vifaranga;
- Maandalizi muhimu kabla ya utunzaji au upokeaji wa
vifaranga yafanyike wiki mbili kabla ya mapokesi ili kuepuka maandalizi ya
haraka haraka
- Endapo chumba au banda lilikuwa ikitumika kutunzia
kuku ni lazima lisafishwe kikamilifu na baada ya usafi huu dawa (disinfectant)
itumike ili kuuwa vimelea vya maradhi ya kuku.
- Weka matandiko kwenye chumba hicho
- Kama vifaranga ni vingi tayarisha mzunguko kwa kutumia
karatasi ngumu isiyozidi urefu wa sentimita 40 endapo kutakuwa na karatasi
ngumu, au kona za chuma kwa kutumia kibao chenye pembe tatu ili vifaranga
visikaliane kwenye kona hizo.
- Endapo utatumia taa ya chemli, taa hiyo isafishwe
masaa 24 kabla ya kulea au kupokea vifaranga taa moja ya chemli unaweza kutunza
vifaranga 50 – 60 kutegemea hali ya hewa ya msimu husika. Endapp jiko la mkaa
litatumika katika utunzaji wa vifaranga hakikisha mkaa umeungua na kutoa moto
mwekundu ili kuepuka hewa yenye sumu mbaya (carbon monoxide) ambayo inaweza
kuua vifaranga. Dalili za sumu mbaya kwenye vifaranga
·
Kupiga kelele ambayo si ya kawaida
·
Vifaranga kulalia
migongo yao
·
Kupata vifo vingi
- Wakati wa kutunza vifaranga ambao huchukua wiki 3 hadi
4 vifo visizidi asilimia 5 endapo vitatunzwa vizuri
- Joto litakiwalo katika utunzaji wa vifaranga ni kama
ifuatavyo.
Wiki ya Nyuzi
joto za centigredi
Kwanza 35
Pili 33
Tatu 31
Nne 29
Lakini kwa kuwa mfugaji hatakuwa na kifaa cha kupimia
joto, mwenendo wa vifaranga kwenye banda ni lazima uangaliwe kwa makini kama
ifuatavyo:-
Vifaranga kusongamana karibu na chanzo cha joto
Hii inaonyesha kwamba joto halitoshi, ongeza taa
Vifaranga kuwa mbali sana na chanzo cha joto
Hii inaonyesha kwamba joto ni kali sana, punguza taa
Vifaranga kuwa upande Fulani tu wa mzunguko hii
inaonyesha upepo unaingia kwenye upande Fulani wa chumba
Funga madirisha au ziba matundu
Kusambaa kwa vifaranga ndani ya mzunguko
Hii inaonyesha joto linatosha na kila kitu kiko sawa
A) Utunzaji wa asili – njia hutumika kwa vifaranga
vichache ambapo temba huachiwa kulea vifaranga vyake. Wakati temba nalea
vifaranga vyake utagaji hukoma
B) Utunzaji kwa kutumia taa- njia hii hutumika endapo
mfugaji atakuwa na vifaranga vingi kwa wakati mmoja. Mfugaji ni lazima awe
makini sana endapo atatumia njia hii.
Ulishaji wa
vifaranga na kuku wanaokua
(i)
Chakula cha kulelea
vifaranga (chick mash) – Chakula hiki kina kiwango cha protini kati ya asilimia
18 hadi 20. Walishwe vifaranga kuanzia wiki ya kwanza hadi ya nane. Uzito wa
Chakula wa kilo 250 unatosha kulisha vifaranga 100 hadi wiki ya nane.
(ii)
Chakula cha kukuzia
(growers mash) – Chakula hiki kina kiwango cha protini kati ya asilimia 13 hadi
15. Walishwe kuku wakuao kuanzia wiki 9 hadi ya 18. Uzito wa Chakula wa kilo
500 unatosha kulisha kuku wakuao hadi kufikia utagaji.
(iii)
Kulisha majani –
kuku wapewe majani kama ya mpapai au luseni baada ya umri wa wiki mbili.
(iv)
Maji safi na salama
– maji safi na salama ni lazima yawepo kwenye kundi la kuku kila mara. Kwani
zaidi ya nusu y uzito wa kuku ni maji. Na maji yasipokuwepo uzito wa kuku
utapungua mno.
Kuanzia siku ya 1 hadi wiki ya
a) 4 kilo 1
b) 8 kilo 4
c) 12 kilo 8.5
d) 20 kilo 8 hadi 12
Nafasi ya eneo la sakafu au ardhi kwa kila kuku:
Wiki 1-4 = 15 x 15 cm
Wiki 5-8 = 30 x 30 cm
Wiki 9-12-45 x 45 cm
UMRI KWA WIKI CHAKULA
KWA KUKU/SIKU
1. Gramu 7 HADI 11
2. Gramu 7 hadi 11
3. Gramu 7 hadi 11
4. Gramu 25 hadi 40
5. Gramu 25 hadi 40
6. Gramu 35 – 45
7. Gramu 35 – 40
8. Gramu 40 – 60
9. Gramu 40 – 60
10. Gramu 40 – 60
11. Gramu 40 – 60
12. Gramu 45 – 70
13. Gramu 45 – 70
14. Gramu 45 – 70
15. Gramu 45 – 70
16. Gramu 60 - 90
17. Gramu 60 – 90
18. Gramu 60 – 90
19. Gramu 60 – 90
20. Gramu 110 – 120 haadi kuuzwa
VYAKULA VITUMIKAVYO
KATIKA UCHANGANYAJI WA VYAKULA VYA KUKU PAMOJA NA VIPIMO VYAKE KWA KILA AINA YA
CHAKULA VYAKULA VITUMIKAVYO:
AINA YA CHAKULA
|
KIWANGO CHA PROTINI (ASILIMIA)
|
KIWANGO CHA JUU CHA KUCHANGANYIA
|
Vyakula vya kutia nguvu mwilini (wanga)
|
|
|
1. Mahindi
|
8-9
|
70%
|
2. Shairi
|
11-16
|
50%
|
3. Ngano
|
12-13
|
70%
|
4. Mpunga
|
7-7.3
|
40%
|
5. Mtama
|
11%
|
30%
|
6. Ulezi
|
13.3
|
30%
|
7. Mhogo
|
2.00
|
30%
|
8. Uwele
|
11-12
|
30%
|
Pumba za – Mahindi
- Ngano
- Mpunga
|
10
12-15
11-12
|
6%
10%
|
Vyakula vya kujenga mwili – protini
A. Protini ya asili ya nyama
1. Dagaa
|
50-70%
|
10%
|
2. Unga wa nyama
|
50-53%
|
10%
|
3. Unga wa nyama na mifupa
|
50-51%
|
10%
|
4. Unga wa damu
|
80%
|
5%
|
5. Maziwa ya unga
|
33-34
|
|
B. Protini ya asili ya mimea
|
|
|
1. Maharage
|
25%
|
30%
|
2. Soya
|
46
|
20%
|
3. Mashudu ya alizeti
|
38-41
|
20%
|
4. ufuta
|
41
|
20%
|
5. mashudu ya pamba
|
50
|
10%
|
6. mashudu ya karanga
|
22.5
|
20%
|
7. mashudu ya nazi
|
20-21
|
2%
|
8. mashudu ya karanga
|
45-46
|
20%
|
Vyakula vitoavyo madini
|
Asilimia ya Kalisiamu (calcium)
|
Asilimia ya Fosforasi (Phosphorous)
|
1. unga wa mifupa
|
23%
|
12%
|
2. Shokaa
|
30%
|
|
3. Magamba ya konokono
|
|
|
4. Dicalcium phosphate
|
24%
|
18%
|
5. Tricalcium phosphate
|
38%
|
19%
|
6. Magamba yamayai
|
|
|
7. chumvi
|
|
|
8. madini kutoka maduka ya dawa
|
|
|
Vyakula vitiavyo vitamin
|
|
|
- lusina iliyosagwa
|
|
2%
|
- luseni iliyosagwa
|
|
2%
|
- unga wa vitamin kutoka madukani
|
|
|
VIPIMO VYA AINA MBALIMBALI VYA VYAKULA
CHAKULA
|
VIFARANGA
|
KUKU WAKUWAO%
|
KUKU WA MAYAI%
|
1. Mahindi yaliyosagwa
|
62.00
|
46.00
|
70
|
2. Pumba za mahindi
|
10.00
|
25.00
|
-
|
3. Mashudu ya pamba
|
10.00
|
10.00
|
10
|
4. Unga wa dagaa
|
6.00
|
2.50
|
3.5
|
5. Mashudu ya alizeti
|
7.00
|
10.50
|
12.00
|
6. Unga wa chokaa
|
2.00
|
2.5
|
1.00
|
7. Dicalcium phosphate
|
1.50
|
1.50
|
1.50
|
8. Chumvi
|
0.50
|
0.50
|
0.50
|
9. Unga wa vitamin
|
1.00
|
1.50
|
1.50
|
jumla
|
100
|
100
|
100
|
Mwongozo: Aina ya vyakula vinavyofanana vinaweza
kutumika endapo kimojawapo hakipatikani.
Mambo ya kufikiria kwanza kabla ya kuchanganya Chakula
cha kuku.
1. Dhumuni la Chakula kwanza kama kuku wa mayai,
vifaranga
2. Chakula vyenyewe vya kuchanganyia
- Je vinapatikana kwenye eneo husika
- Fikiria gharama ya manunuzi ya kila Chakula
- Baadhi ya vyakula vina chembe chembe za sumu
- Urahisi wa usagikaji kwenye tumbo la kuku
- Viini lishe vilivyomo kwenye Chakula husika
3. Matarajio ya kiwango cha uzalishaji
4. Mahitaji ya viini lishe mwilini mwa kuku
5. Urahisi wa vyakula hivyo kuchanyanyika ili kupata
mchanganyiko unaofaa kwa kuku husika
La kuzingatia – Chakula chenye uwezo wa kunyonya unyevu nyevu kiwekwe
mwisho kabla ya kuchanyanya kama vile chumvi. Pia vitamin na baadhi ya madini
yachanyanywe kwanza kwenye pumba au unga uliosagwa au kuparazwa wa nafaka.
Kuku wanahitaji kujengewa banda bora na safi ili wasiathiriwe na madhara
mbalimbali kama wanyama wakali, wezi na mabadiliko ya hali ya hewa. Vile vile
banda bora husaidia kurahisisha kazi ya utunzaji wa kuku, ni muhimu kujenga
banda lenye sifa zifuatazo.
1. Banda lenye kuingiza hewa safi nay a kutosha
2. Banda lenye kuingiza mwanga wa kutosha
3. Banda lenye kuzuia upepo mkali
4. Banda lisilo ruhusu maji kusimama na kuingia ndani na
kwamba imara
5. Banda liwe rahisi kusafishwa
6. Banda liwe na eneo la kutosha kulingana na idadi ya
kuku
7. Banda liwe katika eneo linalofikika kwa urahisi
8. Banda liwe imara na lisiwe la muda mfupi
Vifaa vinavyohitajika katika banda la kuku
Vyombo vya maji vyombo hivi ni kama vya bati, plastiki, madebe, vyungu,
sufuria, vibuyu na magogo yaliyotengenezwa vizuri kwa shughuli husika vyombo
vya maji kwa ajili ya vifaranga na minimum view na kina kidogo kuepuka
vifaranga visizame kwenye maji na kusababisha vifo.
No comments:
Post a Comment