Wednesday, April 1, 2015


1
Ufugaji wa kuku wa Asili
Mwongozo kwa mfugaji
UFUGAJI WA KUKU
WA ASILI
SEHEMU YA KWANZA
2
Ufugaji wa kuku wa Asili
RLDC na Uboreshaji wa Maisha Vijijini
Shirika la Rural Livelihood Development Company (RLDC ni moja ya mafanikio
ya ushirikaiano kati ya Tanzania na Uswisi kwenye mchakato wa kupambana na
umaskini na kuboresha maisha ya jamii za vijijini. Hii ni taasisi isiyo ya kibiashara
ili yoanzishwa mwaka 2005 na mashirika ya Intercooperation na Swisscontact,
lengo kuu likiwa kutekeleza Programu ya kuendeleza maisha ya jamii za vijijini
(RLDP). Programu hii inasha bihiana na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupambana
na Umaskini (MKUKUTA). Dhamira kuu ya RLDC ni Kuendeleza/kuboresha mifu
mo ya masoko ili kuwawezesha wazalishaji wa vijijini kutumia
fursa zilipo kuboresha maisha yao.
Kwa sasa, RLDC inatelekeleza awamu ya pili ya mpango wake (2008-2011)
na inaweka msukumo zaidi kwenye uendelezaji wa mifumo ya masoko. RLDC
inafanya kazi katika mikoa sita ya Kanda ya kati-Dodoma, Singida, Morogoro,
Shinyanga, Tabora, na Manyara. Jamii nyingi maskini zinaishi katika ukanda huu
wenye sehemu kubwa yenye hali ya mvua chache na nusu jangwa inayostawisha
shughuli chache za kiuchumi.
Hata hivyo kuna fursa nyingi sana zinazoweza kutoa ajira na kuboresha ya
jamii zake. RLDC inafadhiliwa na Serikali ya Uswisi kupitia shirika la Uswisi la
maendeleo (SDC).
Kwa sasa RLDC inawezesha sekta za pamba, alizeti, maziwa, ufugaji wa kuku wa
kienyeji, mpunga na habari kupitia vipindi vya redio kwa ajili ya wazalishaji wa
vijijini.
“RLDC inaboresha mifumo ya masoko ili kuwezesha wazalishaji wa
vijijini kuinua maisha yao”
1
Ufugaji wa kuku wa Asili
Sehemu ya Kwanza
Ufugaji wa kuku wa asili kwa ‘Mfumo wa Bariadi’
1.0 Utangulizi
Mwaka 2008/9 RLDC ilifanya majaribio ya mfumo wa ufugaji wa kuku wa asili kupitia
vikundi vidogo vya wafugaji wa vijijini katika vijiji vya Bupandagila na Mbiti, Wilayani
Bariadi katika Mkoa wa Shinyanga. Huu ni ufugaji wa ushirika unaolenga kusaidia
wazalishaji wadogo wa mazao ya kuku. Utaratibu huu unahusisha mgawanyo wa
kazi katika ufugaji ili kurahisisha na kusaidiana majukumu na gharama.
Lengo kubwa la majaribio haya ilikuwa ni kuona kama mfugaji mmoja angepunguziwa
majukumu yake katika uzalishaji ili kuongeza uwezo wake wa uzalishaji. Vijiji husika
vilifanikiwa kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa kuku watano hadi kufikia kuku mia
moja katika miezi michache. Mafanikio ya mradi huu ndio chachu iliyofanya RLDC
kuona umuhimu wa kufundisha na kudurufu mfumo huu katika maeneo mengine
ya nchi na kuweka wazi kwa watu wengine ambao watakuwa tayari kujihusisha na
ufugaji wa kisasa na kibiashara wa kuku wa asili bila usaidizi wa wafadhili.
Mfumo huu unaonyesha nyenzo muhimu zinazolenga kurahisisha ufugaji wa
kuku kwa wafugaji wadogo walioko vijijini kwa kupunguza majukumu ambayo
mtu mmoja angetakiwa kufanya katika mlolongo wa uzalishaji. Mfumo unalenga
katika utendaji wa vikundi vidogo vidogo vinavyopewa mafunzo kulingana na kazi
waliyochagua kufanya katika mlolongo mzima wa uzalishaji. Ufugaji wa namna hii
unamfanya mfugaji awe na sehemu ndogo anayoimudu katika mfumo mzima wa
ufugaji kuku (mfano kikundi kimoja kujihusisha na utotoleshaji wa vifaranga pekee
au utafutaji wa masoko). Mfumo huu pia umeazima baadhi ya mafanikio kutoka
mfumo uliofanyiwa kazi huko Bangladesh na kufanikiwa katika nchi nyingi zikiwemo
za Afrika ya Mashariki.
Licha ya ukweli kwamba mfumo huu unapunguza majukumu, pia unaongeza
uwezekano wa wafugaji kupata huduma zingine muhimu wakiwa katika vikundi.
Huduma hizo ni pamoja na mafunzo, mikopo, uwezekano wa kujifunza kwa pamoja
ujuzi mpya katika ufugaji na hata kuwa na sauti ya pamoja katika soko. Katika kijitabu
hiki utaelezwa zaidi jinsi ya kufanya kazi kupitia mfumo huu wa Bariadi.
2
Ufugaji wa kuku wa Asili
2.0 ‘Mfumo wa Bariadi’
Mfumo huu wa uzalishaji huwaweka wazalishaji katika ushirika au kikundi kimoja
kikubwa cha pamoja chenye taratibu, uongozi na maadili yake. Umoja huu wa
wafugaji husajiliwa kisheria. Viongozi wa kikundi hiki (Kamati kuu ya utendaji ya
kijiji) hutokana na viongozi wa vikundi vidogo vidogo vinavyoundwa na shughuli
wanayoifanya katika uzalishaji (mfano wazalishaji wa chakula, wanaohusika na afya
ya kuku n.k). Mwenyekiti na Naibu Mwenyekiti wa kikundi kidogo ndio wanaounda
uongozi wa kikundi kikubwa (umoja wa wafugaji) cha hapo kijijini.
Mfumo huu wa uongozi unatakiwa kuzingatia uwakilishi mzuri wa vikundi vyote katika
jamii husika ili kuleta uwiano wa utendaji na maamuzi yanayolenga maendeleo ya
vikundi vyote kijijini. Pia mfumo huu unasaidia uratibu wa maendeleo katika sekta
nzima.
Kamati kuu ya
utendaji
Uwakilishi toka
vikundi vidogo
vidogo
Wazalishaji
vifaranga
Watunzaji
wa
vifaranga
Masoko
Wazalishaji
chakula
Kuweka
na
kukopa
Afya ya
kuku
Mfumo wa uongozi wa umoja wa wafuga kuku kijijini
3
Ufugaji wa kuku wa Asili
Kutokana na mafanikio mazuri ya kiutendaji yaliyopatikana huko Baraidi, RLDC
imeamua kushirikisha wadau wengine wa uzalishaji katika wilaya nyingine za
Ukanda wa Kati ili kuendeleza biashara na sekta ya uzalishaji wa kuku wa asili.
Hata hivyo, tumejifunza kuwa mfumo ungeweza kufanya vizuri zaidi kama yafuatayo
yatazingatiwa.
A.
Wafugaji wa kuku wote waliojiunga katika kikundi wawe na umoja wa wafugaji
pale kijijini. Kwa maana ya kwamba sharti mojawapo la kuwepo katika
kikundi ni kuwa mfugaji wa kuku wa asili. Kwa kuanzia, kila mmoja atafuga
kuku wa umri wa mwezi mmoja hadi kufikia kuuzwa kwa wafanyabiashara.
Wafanyabiashara, watengenezaji wa chakula, wauza madawa na watu
wengine wote hawataruhusiwa kuwepo kwenye kikundi ila tu kama watafuga
kuku.
B.
Kila mtu katika umoja wa wafugaji wa kuku anapaswa kuwa katika kundi
mojawapo maalumu katika uzalishaji. Hiyo inamaanisha kuwa kila mfugaji
atakuwa na kazi mbili katika ufugaji; atafuga kuku hadi umri wa kuuza na
atajihusiha na kikundi kidogo kimojawapo katika mzungukuko wa uzalishaji.
Hii itampa nafasi ya kujifunza mambo mengi yahusuyo biashara ya kuku.
Vikundi hivyo vimeganyika kulingana na majukumu kama invyooneshwa
hapa:
Utotoleshaji wa vifaranga
Utunzaji wa vifaranga vya siku moja
Uboreshaji na utunzaji afya ya kuku
Utengenezaji wa chakula cha kuku
Utafutaji wa habari na Masoko ya kuku
Kuweka na kukopa
Makundi mawili ya mwanzo yaweza kuunganishwa kulingana na hali halisi ya wadau.
Utengenezaji wa vikundi mbali mbali utajadiliwa katika mafunzo ya awali ya umoja
wa wazalishaji. Pia hali halisi ya wazalishaji kijijini itajadiliwa kama kuwa na makundi
yote ( mawili ya mwanzo) ama kuwa na kundi moja tu katika hayo.
4
Ufugaji wa kuku wa Asili
3.0 Shughuli za vikundi
3.1.
Kikundi cha watotoleshaji vifaranga
Hiki kitakuwa na jukumu la kulea kuku wazazi wenye sifa inayopendwa
na kikundi na wanaweza kuchanganya mbegu ili kupata kuku bora. Kwa
kuanzia, kikundi kitatumia njia za asili za kutotolesha na baadaye kulingana
na uhitaji kuongezeka waweza kuamua kutumia viatamizi. RLDC kupitia
watendaji wake vijijini itakusanya habari muhimu kuhusu viatamizi na
kuhakikisha habari hizi zinawafikia wahusika wa kikundi.
3.2 .
Kikundi cha Walezi wa vifaranga
Hiki kinahusisha vifaranga wa siku moja hadi wiki tano. Wanakikundi
watawajibika kuchukua vifaranga toka kwa watotoleshaji na kuvilea hadi
kufikia umri tajwa. Wanakikundi watawajibika kuwapa chanjo na madawa
muhimu kulingana na magonjwa yanayojulikana katika eneo husika.
Wanachama wa kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika chanjo na
mahitaji mengine mengi yatakayohitajika kwa ajili ya afya bora ya kuku.
Pia watahitajika kuwekeza katika mabanda mazuri yenye kutunza vifaranga
mbali na maadui mbalimbali na uambukizo wa magonjwa. Baada ya wiki
tano, vifaranga watauzwa kwa wanavikundi wengine watakaowatunza hadi
umri wa kuuzwa au kutunzwa kama kuku wa mbegu. Hata hivyo, wakati wote
wa utunzaji, wanachama watahitaji huduma toka kwa kundi linaloshughulika
na afya ya kuku pamoja na watengenzaji wa chakula.
3.3.
Kikundi kinachohusika na afya ya kuku.
Wanachama wa kikundi hiki watafundishwa namna bora ya kutambua
magonjwa, kuchanja kuku na kutibu magonjwa mbalimbali ya kuku.
Wanachama wa kundi hili watafanya kazi kwa karibu na wataalamu wa
serikali waliopo katika eneo lao ili kuboresha huduma yao pale wanapoona
wanahitaji utaalamu zaidi. Wanachama wa kikundi hiki watalazimika
kuwekeza katika kununua madawa, chanjo na vifaa vya kutunza baridi.
5
Ufugaji wa kuku wa Asili
3.4.
Kikundi cha watengenezaji chakula
Hiki kitahusika na kuchanganya chakula na kusaga kulingana na mahitaji
yaliyopo. Kikundi kitazingatia aina ya vyanzo vya vyakula vinavyopatikana
katika maeneo yao. Chakula kinachochanganywa kitaalamu husaidia
kupunguza muda wa kuku kufikia muda wa kuchinjwa. Wanachama wa
kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika kununua vifaa vya kusagia na
kuchanganya chakula.
3.5.
Kikundi cha masoko
Kikundi kitahusika na kutafuta habari za masoko ndani na nje ya kikundi na
kuwaunganisha wafugaji na wanunuzi mbali mbali toka masoko mengine
kwa bei nzuri. Wanachama wa kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika
gharama za usafiri kwa ajili ya kutafuta masoko.
Chombo cha asili cha kutunza joto – vifaranga
6
Ufugaji wa kuku wa Asili
3.6.
Kikundi cha kuweka na kukopa.
Wanachama wake watasimamia shughuli zote za kuweka na kukopa kwa
wanachama wote wa umoja katika kijiji husika. RLDC imekusudia kutumia na
kufundisha wafugaji mfumo wa kuweka na kukopa unaotumiwa na shirika
la Care International. RLDC haitatoa mtaji wowote ila kupitia mfumo huu,
tunatarajia kwamba vikundi vitajiwekea malengo mahususi ya kuwafanya
wanachama wote waweze kuweka ili wawe na nafasi ya kukopa hapo baade.
Kikundi pia kitajiwekea taratibu mbalimbali za kuweka na kukopa ikiwa ni
pamoja na viwango maalumu na vipindi vya kuweka, kuchukua mkopo
na kurudisha na riba zake. Taratibu zote zitathibitihwa na kupitishwa na
wanachama wote kabla hazijaanza kutumika.
Jedwali hapo chini linaeleza kwa kifupi kila kikundi, majukumu yake, ujuzi unaotakiwa
(ambao kila kikundi kitafundishwa) pamoja na eneo la uwekezaji.
Jina la kikundi
Watotoleshaji
wa vifaranga
Watunzaji wa
vifaranga
Afya ya kuku
Watengeza
chakula
Masoko
Kuweka na
kukopa
Jukumu
Kuku wazazi
Kulea vifaranga
Afya ya kuku
Utengenezaji wa
chakula bora
Habari za
masoko
Kuweka na
kukopa
Ujuzi unaohitajika
Kuku wazazi bora
Matunzo mahususi ya
kuku
Chakula na nyumba bora
Magonjwa ya kuku
Magonjwa
Nyumba za vifaranga
Chakula cha vifaranga
Udhibiti wa magonjwa
Mchanganyiko bora wa
chakula
Madawa na kinga
Matumizi bora ya dawa
na vyakula
Vyanzo bora vya vyakula
Utengenezaji wa chakula
Matumizi sahihi ya
chakula kwa umri
Utafutaji wa masoko
Namna ya kupata habari
za masoko
Namna ya kuweka
kumbukukumbu za
kuweka na kukopa
Eneo la kuwekeza
Kuku bora - wazazi
Nyumba bora zenye
joto mahususi
Vifaa vya kulishia
Chanjo na madawa
Sanduku la kutunzia
dawa (Cold box)
Vyanzo vya vyakula
Vifaa vya
kuchanganyia na
kusagia
Gharama za usafiri
na kupata habari za
masoko
Kuweka na kukopa
7
Ufugaji wa kuku wa Asili
4.0 Uongozi
Kama ilivyoelezwa hapo juu, kila kikundi kidogo kitachagua mwenyekiti na naibu
mwenyekiti kutoka kwa wanachama wake. Umoja wa wafugaji kama kikundi kikuu
cha wafugaji watachagua mwenyekiti na naibu katibu wake ambao hatakuwa
na madaraka katika vikundi wanavyotoka. Viongozi wa vikundi (Mwenyekiti na
naibu wake) watatengeneza kamati kuu ya uongozi wa ushirika na watakutana
kadiri inavyohitajika na mujibu wa makubaliano ya mipango ya kikundi. Kamati ya
utendaji itapokea taarifa toka kwa viongozi wa kila kikundi ni kitakuwa na maamuzi
ya mwisho katika umoja. Kamati hii itakuwa na maauzi juu ya usafirishaji wa kuku
ndani ya umoja. Pia kamati itafanya maamuzi juu ya bei za:
Vifaranga wa siku moja
Vifaranga wa wiki tano
Dawa, chanjo na huduma zake
Chakula cha kuku
Changizo la huduma ya masoko ya pamoja
Taratibu zote na riba za mikopo
Kumbuka kwamba; wanachama wa kila kikundi watafundishwa kulingana na mahitaji
ya utendaji wao. Wanachama wote watapatiwa vitini vya kila somo wanalofundishwa
kwa ajili ya kumbukumbu zao.
8
Ufugaji wa kuku wa Asili
5.0 Mwisho
RLDC inatarajia kuwa mfumo huu utaleta manufaa makubwa kwa wafugaji wa kuku
wa asili kwa kubadilisha mfumo holela wa ufugaji ili kupata kuku bora, wenye bei nzuri
katika soko na idadi inayoweza kutegemewa kila wanapohitajika. Pia tunaamini kuwa
mfumo wa masoko utaboreshwa kwani kila mtu atajishughulisha na jukumu moja
analoweza kulimudu vizuri kwa muda muafaka. Ongezeko la kuku bora linatarajiwa
kuongeza ulaji wa kuku mijini na vijijini na hivyo kuboreha afya za walaji kwa kupata
protini nyingi zaidi. Hali hii inatarajiwa kuongeza kipato kwa wafugaji wa kuku wa
vijijini na hivyo kuoboresha maisha yao. Serikali pia inatarajiwa kunufaika na mfumo
huu kwani mapato kupitia kodi mbalimbali yataongezeka. RLDC inatamani kuona
wadau wa kuku wa asili wanaweza kuuza kuku katika masoko makubwa ya ndani na
nje ya nchi.
9
Ufugaji wa kuku wa Asili
10
Ufugaji wa kuku wa Asili
Jengo la NBC
Ghorofa ya Pili, Mtaa wa Nyerere
S.L.P. 2978, Dodoma, Tanzania.
Simu +255 26 2321455, Faksi +255 26 2321457.
Barua pepe: info@rldc.co.tz.
Tovuti: www.rldc.co.tz.

No comments:

Post a Comment